Tuesday, December 09, 2014

TRA KUCHAMBUA RIPOTI YA KITUO CHA UTAFITI CHA KODI CHA KIMATAIFA (ICTD)

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade, kushoto akiwa na afisa mtendaji mkuu wa kituo cha kimataifa cha kodi na maendeleo, Prof Mick Moore, wakiongoza majadiliano juu ya mada mbalimbali zilizowasilishwa katika mkutano mkuu wa mwaka wa kituo cha kimataifa cha kodi na maendeleo,mkutano uliofanyika jana jijini Arusha
 Wataalamu wa kimataifa  wa masuala ya kodi  wakiendesha mjadala katika mkutano wa mwaka wa kituo cha kimataifa cha utafiti wa masuala ya kodi,mkutano uliofanyika jana  jijini Arusha ,Kamishna Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato Uganda (URA), Milly Nalukwago (kushoto), Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade (katikati) na  Mtaalam wa Kodi wa Uingereza, Rhiannon Mc Cluskey.
Kamishna mkuu wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA RISHED BADE kushoto akiwa na afisa mtendaji mkuu wa kituo cha kimataifa cha kodi na maendeleo Prof MICK MOORE wakiongoza majadiliano juu ya mada mbalimbali zilizowasilishwa katika mkutano mkuu wa mwaka wa kituo cha kimataifa cha kodi na maendeleo,mkutano uliofanyika jana jijini Arusha

Mwakilishi  wa Channel Ten Arusha, Jamila Omar (katikati) , Mwakilishi wa kituo cha Star TV Arusha, Ramadhani Mvungi ,Iddy Uwesu wa Azam tv Arusha wakifanya mahojiano maalumu na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA)  Rished Bade jijini Arusha wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa kituo cha kimataifa cha kodi na maendeleo.
 ***********
Mamlaka ya mapato nchini TRA imeanza kuchambua ripoti ya utafiti uliofanywa na kituo cha kimataifa cha utafiti wa masuala ya kodi na maendeleo inayobainisha changamoto mbalimbali za ulipaji kodi katika
maendeo mbalimbali nchini.

Zoezi la uchambuzi wa ripoti hizo linatajwa kuwa na shabaha ya kuangalia mapungufu yaliyopo na kuboresha mifumo ya sheria na ulipaji kodi kwa hiari.

Sehemu ya Taarifa ya utafiti uliofanwa katika kipindi cha mwaka uliopita na kituo cha kimataifa cha kodi na  maendeleo katika mikoa mbalimbali nchini, inabainisha mazingira tofauti ya ulipaji wa kodi ambapo baaadhi ya maeneo yameonekana kuwa katika changamoto kubwa za ukwepaji kodi.

Kamishana wa TRA Rished Bade kizungumza Jijini Arusha wakati wa Mkutano wa kimataifa baina yao na kundi la wataalamu, wanaofanya utafiti kuhusu masuala ya kodi duniani amesema pamoja na mapitio ya ripoti za utafiti wa taasisi hiyo,fursa hiyo inatoa mwanya kwa wataalamu wa ndani kujifunza mbinu za kushughulikia changamoto za walipa kodi wanaofanya biashara za kimataifa.

Awali Afisa Mtendaji Mkuu wa kituo cha kimataifa cha kodi na maendeleo Profesa Mick Moore ameeleza kusudio la tafiti zao katika nchi mbalimbali za Afrika kuwa unalenga kuimarisha mifumo ya kodi hususani katika sekta za maliasili zikiwemo Madini,Gas na Mafuta.

Katika hatua nyingine Mamlaka ya mapato nchini TRA imeibuka kinara kwa kuwa na hesabu bora miongoni mwa taasisi za serikali kwa mwaka 2013-2014 zinazotolewa na bodi ya wahasibu na wakaguzi wa hesabu nchini NBAA ambapo kamishna wa mamlaka hiyo akizungumza Jijini hapa katika hafla ya kukabidhiwa ushindi huo amesema hatua hiyo inazidi kuwajengea imani walipa kodi juu ya utendaji wa chombo hicho.

Raha tele tabu ya nini?: zinaonyesha ongezeko la idadi ya walipa kodi chini,idadi iliyopo sasa inatajwa kuwa ndogo kulinganisha na mataifa mengine kutokana na mfumo wa kibiashara usio rasmi unaopelekea kupunguza idadi ya walipa kodi wanaofikia milioni moja nukta nane hivi sasa.

ASKOFU DESMOND TUTU ANA TEZI DUME


Askofu mstaafu Desmond Tutu
Askofu mkuu mstaafu wa Cape Town,Desmond Tutu,ameahirisha mipango ya ziara zake kwa mwaka mzima ujao kutokana na sababu za kiafya.

Taarifa iliyotolewa na taasisi yake imeeleza kuwa Askofu huyo ataanza matibabu hivi karibuni ili kukabiliana na tezi dume ambayo amedumu nayo miaka kumi na mitano iliyopita.


Binti wa Askofu huyo amemuelezea baba yake mwenye umri wa miaka themanini na miwili,kwamba hatahudhuria tuzo za Nobel zitakazo fanyika baadaye wiki hii huko Rome, Italia.

Haya ndiyo makubwa yaliyoandikwa na Magazeti ya Tanzania leo Desemba 10

.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

MATOKEO YA LIGI YA MABINGWA ULAYA!!!

article-2867609-23EC051900000578-81_636x382
Michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya imeendelea usiku huu ikiwa kwenye mzunguko wake wa mwisho wa hatua ya makundi .
Katika michezo iliyopigwa hii leo timu ya Arsenal toka England ilifanikiwa kushinda kwenye mchezo wake dhidi ya Galatasaray ya Uturuki kwa matokeo ya 2-4 katika mchezo uliopigwa huko Istanbul.
Kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey akiifungia timu yake katika ushindi wa 2-4 dhidi ya Galatasaray.
Kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey akiifungia timu yake katika ushindi wa 2-4 dhidi ya Galatasaray.
Arsenal ilifunga mabao yake kupitia kwa Aaron Ramsey na mshambuliaji raia wa Ujerumani Lukas Podolski ambapo kila mmoja alifunga mabao mawili .
Katika mchezo mwingine wa kundi D wawakilishi toka ujerumani Borrusia Dortmund walibanwa mbavu wakilazimishwa sare ya 1-1 katika mchezo dhidi ya Anderlecht ya Ubelgiji.
Matokeo haya yanamaanisha kuwa timu za Arsenal na Borrusia Dortmund zimefanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora ambapo Dortmund wamefuzu kama washindi huku Arsenal wakishika nafasi ya pili .
Katika michezo mingine iliyochezwa usiku huu Real Madrid walifanikiwa kushinda mchezo wao wa 19 mfululizo katika mashindano yote wakiwafunga Ludogorets toka Bulgaria 4-0 .
23EB782B00000578-0-image-a-28_1418159216142
Wafungaji wa Real kwenye mchezo huo walikuwa Cristiano Ronaldo , Gareth Bale , Alvaro Arbeloa na Alvaro Medran .
Ushindi huu umewafanya Real wafuzu hatua ya 16 bora kwa kishindo wakiwa wamekusanya pointi 18 baada ya kushinda michezo yote 6 ya kundi lao .
Liverpool ambayo ilikuwa nyumbani ikicheza na Fc Basle iliambulia sare ya 1-1 matokeo ambayo yalikuwa na faida kwa wapinzani wao ambao wanaungana na Real Madrid kufuzu hatua ya kwanza ya mtoano.
Fc Basle imewatoa Liverpool kwenye michuano ya ligi ya mabingwa baada ya kuwalazimisha sare ya 1-1.
Fc Basle imewatoa Liverpool kwenye michuano ya ligi ya mabingwa baada ya kuwalazimisha sare ya 1-1.
Katika michezo mingine Juventus na Atletico Madrid walitoka sare ya bila kufungana , Olympiakos wakawafunga Malmo 4-2 , Benfica na Bayer Leverkusen nazo zikatoka sare ya 0-0 , huku As Monaco ikishinda dhidi ya Zenith St Petersburg kwa matokeo ya 2-0 .
Kwa matokeo haya timu za Juventus , Atletico Madrid , Monaco na Bayer Leverkusen zinaungana na Arsenal , Dortmund , Real Madrid na Fc Basel kufuzu hatua ya 16 bora .
sare ya 1-1 dhidi ya Atletico Madrid ilitosha kuwavusha Juventus kwenye hatua ya 16 bora.
sare ya 1-1 dhidi ya Atletico Madrid ilitosha kuwavusha Juventus kwenye hatua ya 16 bora.

MAITI ZA FAMILIA 5 ZAZIKWA KWENYE KABURI MOJA..CHEKI TUKIO ZIMA HAPA

Maiti za aila moja zazikwa kwa kaburi la pamojaBIWI la simanzi lilitanda JANA Jumanne katika kijiji cha Kimuchu, eneo la Juja, Kaunti ya Kiambu, wakati wa mazishi ya watu watano wa familia moja waliokufa katika hali ya kutatanisha.
Jamaa za marehemu Paul Magu, 35, mkewe Lydia Wangui, 35 na watoto wao Allen Muhiu (9), Ryan Ndau (8) naTiffany Wambui (5) walishindwa kuzuia machozi na baadhi yao kuzirai wakati wa mazishi hayo.

Kasisi James Kamura wa Kanisa la Kiangilikana Thika, alitoa mahubiri yaliyogusa wengi huku akiitaka serikali iwaadhibu waliowaua watoto hao na mama yao.

“Ni jambo lenye uchungu sana kwa familia kuweza kuvumilia. Ni vigumu kuelewa kilichotendeka kwa sababu wote wamekufa. Damu ya binadamu haifai kumwagwa kama ya mnyama,” akasema Kamura.

Magu aligongwa na basi kwenye barabara ya Thika-Garissa nao mwili wa mkewe uliokuwa na majeraha ukapatikana karibu na hoteli ya Paradise Lost Resort, Kiambu.

Miili ya watoto wao ilipatikana kichakani siku chache baadaye karibu Tatu City, eneo la Ruiru.

Jumanne, miili ya familia hiyo ilipelekwa eneo la mazishi kwa magari matatu ya kubebea maiti kisha ikapelekwa kwenye kaburi la pamoja ambapo ilizikwa.

Waombolezaji kadha walizirai na kuondolewa eneo la mazishi.

“Haiwezekani kwamba mauaji haya yalitekelezwa na mtu mmoja. Kuna watu walio hai waliohusika na uhalifu huu wa kikatili na ni lazima serikali ichukue hatua,” akasema Kasisi Kamura akiongoza ibada ya wafu katika nyumba ya wazazi wa Magu, karibu na mji wa Thika.

Wakazi walifika kwa wingi kwa ibada na mazishi ambayo yalihudhuriwa na viongozi wa eneo hilo wakiongozwa na Mbunge wa Juja Francis Munyua. Gavana wa Kiambu William Kabogo aliwakilishwa na msaidizi wake Sammy Onyango.

Kukatiza ibada
Mhubiri alilazimika kukatiza ibada mara kadha na kuomba jamaa waliolemewa na huzuni wasaidiwe.
Wazazi wa mama ya watoto hao, Francis Ndau na Mary Muthoni na jamaa zao wa karibu kutoka Kaunti ya Nyandarua walishindwa kusimama wakati wa kuimba kwa kulemewa na majonzi.
Kasisi aliwagusa zaidi waombolezaji aliposimulia matukio yaliyotangulia kupatikana kwa miili ya watoto hao siku chache baada ya wazazi wao kufa katika hali ya kutatanisha.  

“Mimi binafsi niliomba watoto hao wapatikane wakiwa hai. Lakini nililia walipopatikana wamekufa. Kwa nini mtu afanye hivi,” akashangaa.

Kasisi Kamura alisema mauaji hayo yalihusu imani na kuwataka polisi wachunguze kilichotendeka.

“Wakenya wana haki ya kujua yanachofunza mashirika ya kidini na vitendo vyake na ni jukumu la serikali kuwaondoa wahubiri wanaopotosha,” akasema.

Aliongeza kuwa wakati umefika kwa serikali kudhibiti mashirika ya kidini kwa sababu vitendo vya baadhi yake ni vya kutiliwa shaka.
Aliwataka wafuasi wa makanisa wakatae baadhi ya wahubiri wanaotumia dini kujitajirisha.

Sunday, December 07, 2014

Ndege iliyobeba silaha yakamatwa Nigeria

Halikopta mbili za kijeshi ni miongoni mwa zana za kivita zilizokamatwa kwenye ndege hizo ya mizigo.
Ndege ya mizigo iliyosheheni silaha za kivita imekamatwa katika uwanja wa ndege wa Kano nchini Nigeria.

Licha ya kukanusha awali, Urusi imesema inamiliki ndege ya mizigo iliyozuiwa katika uwanja wa ndege wa Kano kaskazini mwa Nigeria baada ya kugunduliwa imebeba silaha ambazo hazikuwa zimearifiwa.
Hata hivyo, Msemaji wa Ubalozi wa Urusi nchini Nigeria, ambaye aliliambia Shirika la Habari la Urusi TASS kwamba wanamiliki ndege hiyo, amesema silaha hizo ni za kikosi cha kulinda amani cha Ufaransa.
Kwa mujibu wa Mwandishi wa habari wa BBC ndege hiyo bado inashikiliwa uwanjani hapo.
Awali, msemaji wa kikosi cha kulinda amani cha Ufaransa katika Jamhuri ya Afrika ya kati aliiambia BBC kwamba hawafahamu chochote kuhusu helikopta mbili, magari ya kijeshi na silaha nyingine zilizokuwa katika ndege hiyo.

Hata hivyo baadaye alipiga simu kufuta usemo wake kwa kusema kuwa ndege hiyo ilikuwa imebeba silaha kwa ajili ya wanajeshi wao, walioko katika kambi ya N’damena, ambazo zitapelekwa baadaye Ufaransa.
Msemaji wa Ubalozi wa Urusi mjini Abuja alisema pia ndege hiyo ni yao. Akitatanisha taarifa aliyoitoa awali kwamba ndege hiyo si yao.
Kwa nini Ufaransa inatumia ndege ya Urusi kubeba silaha zake? na kwa nini ilisimama katika uwanja wa Kano, wakati ikiwa inaelekea nchi jirani ya Chad na hata Cameroun ikitokea Afrika ya kati? Kwanini baadhi ya silaha hazikuorodheshwa katika ndege hiyo kama zimebebwa?.

Hayo ni maswali yalioulizwa pande zote.
Seriakli ya Nigeria ambayo ndio muhusika mkuu wa tukio hilo, haijasema chochote.
Baadhi ya wachambuzi wanasema Nigeria inamiliki silaha hizo ilizonunua katika soko haramu. Wengine wanasema silaha hizo zilinunuliwa kutoka kwa waasi wa Seleka katika Jamhuri ya Afrika ya kati, wakielezea kwanini ndege hiyo imeingia nchini humo kutoka mji mkuu wa nchi hiyo, Bangui.
Nigeria imewekewa vikwazo vya silaha kutoka Marekani na nchi hiyo imekuwa ikiarifiwa kutumia njia zisizo halali kupata silaha kwa ajili ya kupambana na wapiganaji wa Boko haram.

MAANDALIZI YA SIKU YA UHURU YALIVYOPAMBA MOTO!


Majeshi ya ulinzi na usalama yakitoa salamu katika mazoezi.
Vijana wa halaiki wakionyesha ufundi wao.
Vikundi mbalimbali vya ngoma, kwaya na ‘brass band’ vikionyesha sanaa yao.
Baadhi ya wadau waliohudhuria mazoezi hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)MAANDALIZI ya siku ya uhuru wa Tanganyika (Tanzania Bara) Desemba 9, kutimiza miaka 53, yanaendelea Uwanja wa Uhuru ambapo kutakuwa na gwaride la kijeshi vikundi vya sanaa, kwaya, halaiki ya vijana, ‘brass band’ na matarumbeta.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, amesema milango katika Uwanja wa Uhuru itakuwa wazi kuanzia saa 12:00 asubuhi ambapo wananchi watakaofika katika hafla hiyo watatumia mlango wa kusini upande wa Barabara ya Mandela kuingia uwanjani, na waalikwa wenye kadi watatumoa mlango wa geti namba mbili 2 na viongozi watatumia geti namba tatu 3.

Recent Posts


Unordered List