![]() |
Mtanzania Idris |
Mshiriki wa Tanzania ndani ya mjengo wa Big Brother ‘hotshots’ , Idris Sultan ndiye ameibuka kidedea leo usiku katika shindano hilo huko Afrika Kusini Baada ya siku 63 za msimu wa 9 .
Idris amekuwa Mtanzania
wa pili kushinda shindano hilo, baada ya Richard Dyle Bezuidenhout kuibuka
kidedea mwaka 2011 katika Big Brother Afrika II.
Baada ya siku 63
jumba hilo lilikuwa limebakiza washindani Sipe, Nhlanhla, Mackey 2, JJ, Idris,
Mam’bea, Butterphly na Tayo — kati ya washiriki 26.Watu hao katika fainali waliondoka kwa namna hii: Butterphly na Mam’bea, JJ na Sipe, Nhlanhla na Macky2, wakiwaacha Idris na Tayo.
Kwa ushindi huo Braza Idris anaondoka na kitita cha dola za Marekani 300, 000. Chezea Bongo wewe!
0 comments:
Post a Comment