Friday, September 26, 2014

IBARA 28 ZA WARIOBA ZILIZOFUTWA!!!


IMG_4409 Na Sharon Sauwa na Julius Mathias, Mwananchi
Ijumaa,Septemba26 2014
Ibara ya 15 iliyokuwamo katika Rasimu ya Warioba ilisema: “Kiongozi wa umma wakati anapotekeleza shughuli za kiserikali, akipewa zawadi, zawadi hiyo itakuwa ni mali ya Jamhuri ya Muungano na ilitaka Bunge kutunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo mengine, thamani, kiwango, aina na uhifadhi wa zawadi kwa Jamhuri ya Muungano. Mbali na ibara hiyo, pia Ibara ya 16 iliyohusu ufunguaji akaunti nje ya nchi, imeondolewa.
Katiba Mpya: Ni mchezo wa namba
Dar/Dodoma. Rasimu ya Katiba inayopendekezwa iliyowasilishwa bungeni juzi, imeondoa Ibara 28 zikiwamo zinazowataka viongozi wa umma kutopokea zawadi kwa manufaa yao binafsi wala kufungua akaunti ya benki nje ya nchi pasipo sababu maalumu, Mwananchi limebaini.
Ibara ya 15 iliyokuwamo katika Rasimu ya Warioba ilisema: “Kiongozi wa umma wakati anapotekeleza shughuli za kiserikali, akipewa zawadi, zawadi hiyo itakuwa ni mali ya Jamhuri ya Muungano na ilitaka Bunge kutunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo mengine, thamani, kiwango, aina na uhifadhi wa zawadi kwa Jamhuri ya Muungano. Mbali na ibara hiyo, pia Ibara ya 16 iliyohusu ufunguaji akaunti nje ya nchi, imeondolewa.
Ibara nyingine zilizoondolewa ni pamoja na ya 17 iliyopendekeza uwazi wa mali ikimtaka kiongozi wa umma kutangaza thamani ya mali na madeni yake mara tu baada ya kupata uongozi.
Pia Ibara ya 129 iliyokuwa inawaruhusu wananchi kumvua madaraka mbunge ambaye atashindwa kuwasilisha au kutetea kwa dhati hoja zinazotokana na kero za wapigakura wake au ataacha kuishi au kuhamisha makazi yake kutoka eneo la jimbo la uchaguzi kwa zaidi ya miezi sita bila sababu za msingi imeondolewa.
Ibara 28 zilizoondolewa
15. (1) Kiongozi wa umma wakati anapotekeleza shughuli za kiserikali, akipewa zawadi, itakuwa ni mali ya Jamhuri ya Muungano na ataiwasilisha kwa Katibu Mkuu Kiongozi kupitia kwa katibu mkuu wa wizara au kiongozi wa taasisi ya Serikali inayohusika, akiainisha:
(a) aina ya zawadi; (b) thamani ya zawadi; (c) sababu ya kupewa zawadi; na (d) mtu au mamlaka iliyotoa zawadi hiyo.
(2) Neno “zawadi” kama lilivyotumika katika ibara hii linajumuisha kitu chochote chenye thamani atakachopewa kiongozi wa umma katika utekelezaji wa shughuli za umma.
(3) Bunge litatunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo mengine, thamani, kiwango, aina na uhifadhi wa zawadi kwa Jamhuri ya Muungano.
16. Kiongozi wa umma-
(a) Hatafungua au kumiliki akaunti ya benki nje ya Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kwa namna ambayo sheria za nchi zinaruhusu; na (b) hataomba au kupokea mkopo au faida yoyote kwa namna au mazingira ambayo yanashusha hadhi au heshima ya utumishi wa umma.
17.-(1) Kiongozi wa umma atalazimika kutangaza na kuwasilisha, ndani ya siku thelathini baada ya kupata uongozi na baada ya kuacha uongozi, mali na thamani yake na madeni yake katika Tume ya Maadili ya Uongozi na Uwajibikaji.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ndogo ya (1), Kiongozi wa umma atalazimika kutangaza na kuwasilisha taarifa ya mali na madeni: (a) yake binafsi; (b) ya mwenza wake wa ndoa; na (c) ya watoto wake walio chini ya umri wa miaka kumi na nane, mara moja kila mwaka kwa Tume ya Maadili ya Uongozi na Uwajibikaji.

(3) Bunge litatunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo mengine: (a) ngazi au orodha ya viongozi wa umma wanaopaswa kutangaza mali na madeni yao; na (b) utaratibu wa kuwasilisha taarifa ya mali na madeni kwa Tume ya Maadili ya Uongozi na Uwajibikaji kwa mujibu wa Katiba hii.
18.-(1) Kiongozi wa umma hatashiriki katika kufanya uamuzi wa jambo au shughuli yoyote ambayo ana masilahi nayo yeye binafsi, mwenza wake, mtoto wake, jamaa yake, rafiki au mtu yeyote wa karibu.
(2) Kiongozi wa umma hatazungumzia kitu chochote katika Baraza la Mawaziri, Bunge, Kamati au chombo kingine chochote rasmi ambacho ana masilahi nacho ya moja kwa moja au vinginevyo, isipokuwa tu kama atatoa taarifa ya mgongano huo wa masilahi katika chombo hicho.
(3) Itakuwa ni marufuku kwa kiongozi wa umma kushiriki katika uamuzi unaohusu kuongeza au kuboresha masilahi kwa namna yoyote ile yanayohusu wadhifa alionao na endapo atashiriki, basi masharti hayo mapya yataanza kutumika kwa kiongozi wa umma atakayekuja baada ya kiongozi husika kuondoka au kumaliza muda wa kukaa katika nafasi ya madaraka iliyompatia fursa ya kushiriki katika kuamua masilahi husika.
(4) Masharti ya ibara ndogo ya (3), hayatamhusu kiongozi wa umma ambaye kutokana na asili ya nafasi ya madaraka au aina ya kazi zake anapaswa kushiriki katika upangaji wa mishahara au maslahi mengine ya watumishi wa umma.
(5) Kiongozi wa umma hataruhusiwa kushika nafasi za madaraka zaidi ya moja au kutumikia mihimili ya dola zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja.
19. Kiongozi wa umma hataruhusiwa kutumia au kuruhusu kutumika kwa mali yoyote ya umma, zikiwemo zilizokodishwa kwa Serikali, kwa madhumuni ya kujipatia yeye binafsi au kumpatia mtu mwingine manufaa yoyote.
20.-(1) Bunge litatunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo mengine:
(a) utaratibu wa utwaaji wa mali za viongozi wa umma zilizopatikana kwa kukiuka sheria;
(b) utaratibu wa kumwajibisha kiongozi wa umma aliyekiuka maadili na Miiko ya Uongozi; na
(c) uanzishaji wa mitalaa inayohusu Katiba, maadili na uraia, shuleni na vyuoni.
(2) Masharti yaliyoainishwa katika sehemu hii ya Sura ya Tatu yatatumika pia kwa watumishi wa umma baada ya kufanyiwa marekebisho stahiki.

63. Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali ya Jamhuri ya Muungano na kwa ajili ya mgawanyo wa madaraka juu ya shughuli hizo baina ya vyombo vilivyotajwa katika Ibara ya 61, Serikali ya Jamhuri ya Muungano itakuwa na mamlaka juu ya mambo ya Muungano kama yalivyoorodheshwa katika Nyongeza ya Katiba hii. Nchi Washirika.
64.-(1) Kwa mujibu wa Katiba hii, Nchi Washirika ni Tanganyika na Zanzibar.
(2) Serikali ya Tanganyika itakuwa na mamlaka juu ya mambo yote yasiyo ya Muungano yanayohusu Tanganyika.
(3) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itakuwa na mamlaka juu ya mambo yote yasiyo ya Muungano yanayohusu Zanzibar.
(4) Nchi Washirika zitatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia masharti ya Katiba hii na Katiba zao.
(5) Nchi Washirika zitakuwa na hadhi na haki sawa ndani ya Jamhuri ya Muungano na zitatekeleza majukumu yao kwa mambo yote yasiyo ya Muungano katika mamlaka ya Nchi Washirika kwa mujibu wa masharti yatakayowekwa na Katiba za Nchi Washirika.
67.-(1) Kila Nchi Mshirika itateua Waziri Mkaazi atakayeratibu na kusimamia mahusiano baina ya Serikali za Nchi Washirika na kati ya Serikali ya Nchi Mshirika na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Mawaziri Wakaazi watakuwa na ofisi zao na watafanya kazi wakiwa Makao Makuu ya Serikali ya Muungano.
(3) Pamoja na majukumu mengine watakayopangiwa na Serikali za Nchi Washirika, Mawaziri Wakaazi watakuwa na majukumu yafuatayo:
(a) kushughulikia mambo yasiyo ya Muungano yanayohusu ushirikiano au uhusiano wa kimataifa; na
(b) kuwa kiungo baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali za Nchi Washirika na baina ya Serikali za Nchi Washirika.
68.-(1) Serikali ya Jamhuri ya Muungano itapata mamlaka yake kutoka kwa wananchi kupitia uchaguzi wa kidemokrasia utakaoendeshwa na kusimamiwa na chombo kitakachopewa mamlaka na Katiba hii, na vilevile, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zitapata mamlaka kupitia uchaguzi wa kidemokrasia utakaoendeshwa na kusimamiwa na vyombo vitakavyopewa mamlaka chini ya Katiba zao.

(2) Serikali za Nchi Washirika, katika kutekeleza mamlaka zao, zitawajibika kustawisha mamlaka ya wananchi kwa kugatua madaraka kwa serikali za mitaa zitakazoanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Tanganyika au Katiba ya Zanzibar, kama itakavyokuwa.
99.-(1) Kutakuwa na Waziri Mwandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano atakayeteuliwa na Rais na kuthibitishwa na Bunge.
(2) Waziri Mwandamizi kabla ya kushika madaraka yake, ataapa mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na kiapo kingine chochote kama itakavyoelezwa na sheria za nchi.
(3) Mtu anaweza kuteuliwa kuwa Waziri Mwandamizi endapo atakuwa na sifa zilizoainishwa katika Ibara ya 101.
(4) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, Waziri Mwandamizi atashika madaraka ya Waziri Mwandamizi hadi:
(c) siku ambapo Rais mteule ataapa kushika madaraka ya urais; au
(d) siku ambapo atafariki dunia akiwa katika madaraka; au
(e) siku atakapojiuzulu; au
(f) siku ambapo Rais atakapomteua mtu mwingine kushika madaraka ya Waziri Mwandamizi.
100.-(1) Waziri Mwandamizi atakuwa na madaraka ya udhibiti na usimamizi wa utekelezaji wa shughuli za Serikali za siku hadi siku.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, Waziri Mwandamizi atatekeleza majukumu yote atakayoelekezwa na Rais na katika utekelezaji wa majukumu yake atawajibika kwa Rais.
103.-(1) Mawaziri na Naibu Mawaziri hawatakuwa na haki ya kuhudhuria vikao vya Bunge isipokuwa tu:

(a) endapo kutakuwa na hoja mahususi ambayo Bunge linahitaji ufafanuzi kwa waziri husika; au
(b) endapo Serikali au waziri ataomba na kuruhusiwa kuwasilisha au kuitolea ufafanuzi hoja yoyote Bungeni.
(2) Kwa madhumuni ya ibara ndogo ya (1), waziri atakayeruhusiwa kuhudhuria kikao cha Bunge anaweza kulihutubia Bunge.
(3) Serikali ya Jamhuri ya Muungano, chini ya mamlaka ya Rais, ndiyo itakuwa na uwezo wa kufanya uamuzi juu ya sera za Serikali kwa jumla.
(4) Kila waziri atahudhuria vikao vya Kamati za Bunge kila atakapohitajika na kutoa maelezo au ufafanuzi wa suala lolote linalohusu utendaji katika nafasi ya madaraka yake.
(5) Kwa kuzingatia masharti mengine ya jumla ya Katiba hii, mawaziri watatoa maelezo au taarifa ambazo zinahitajika kutolewa bungeni kwa mujibu wa sheria za nchi.
106.-(1) Kutakuwa na Makatibu Wakuu watakaoteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watumishi waandamizi katika utumishi wa umma kama watakavyopendekezwa na Tume ya Utumishi wa Umma.
(2) Kila Katibu Mkuu atakuwa kiongozi na Mtendaji Mkuu wa Wizara ya Serikali aliyopangiwa na Rais na atashika nafasi ya madaraka ya Katibu Mkuu na kutekeleza majukumu yake kama itakavyoainishwa katika sheria za nchi.
(3) Rais anaweza, kwa mapendekezo ya Tume ya Utumishi wa Umma, kumteua mtumishi mwandamizi katika Utumishi wa Umma kuwa Naibu Katibu Mkuu.
(4) Kila Katibu Mkuu atakuwa mshauri wa mwisho kwa Waziri kwa masuala yote ya utendaji na atatoa ushauri kwa Baraza la Mawaziri katika vikao na kamati zitakazoitishwa na Katibu wa Baraza la Mawaziri.
(5) Katibu Mkuu au Naibu Katibu Mkuu hatashika madaraka yake hadi awe ameapa mbele ya Rais kiapo cha utii na uaminifu au kiapo kingine chochote kinachohusu utendaji wa kazi zake kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria za nchi.
107. Kutakuwa na Kamati Maalum ya Makatibu Wakuu itakayoongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi ambayo itakuwa na majukumu ya kuchambua na kulishauri Baraza la Mawaziri juu ya masuala mbalimbali kabla ya kuwasilishwa na kufanyiwa uamuzi na Baraza hilo na itatekeleza majukumu mengine kama itakavyopangiwa na Baraza la Mawaziri.

112.-(1) Kutakuwa na Sekretarieti ya Tume ya Uhusiano na Uratibu wa Serikali itakayoongozwa na Katibu akisaidiwa na Naibu Katibu ambao watateuliwa na Rais.
(2) Mtu atateuliwa kuwa Katibu au Naibu Katibu ikiwa ana sifa zifuatazo:
(a) ni mtumishi mwandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano au Serikali za Nchi Washirika;
(b) ana shahada kutoka chuo cha elimu ya juu kinachotambulika kwa mujibu wa sheria za nchi; na
(c) ana mwenendo usiotiliwa shaka na jamii.
(3) Katibu na Naibu Katibu watawajibika kwa Tume na watafanya kazi na kutekeleza majukumu ya Sekretarieti.
(4) Uteuzi wa Katibu na Naibu Katibu wa Tume utafanywa kwa kuzingatia msingi kwamba endapo Katibu atateuliwa kutoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano, basi Naibu Katibu atateuliwa kutoka upande wa pili wa Jamhuri ya Muungano.
120.-(1) Bunge litatumia madaraka yake ya kutunga sheria kwa kujadili na kupitisha Muswada wa Sheria ambao utawekwa saini na Rais.
(2) Bila kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (3), Muswada wa Sheria unaweza kuandikwa na Serikali, Kamati ya Bunge au kikundi cha Wabunge.
(3) Wakati wa kuandaa Muswada wa Sheria kuhusu jambo lolote la Muungano, Serikali ya Jamhuri ya Muungano itahakikisha kwamba inawashirikisha wananchi kwa ajili ya kupata maoni na mapendekezo juu ya muswada huo.
(4) Muswada wa sheria utahesabiwa kuwa umepitishwa na Bunge iwapo utaungwa mkono kwa kura za wabunge wasiopungua theluthi mbili ya wabunge wote kutoka Tanganyika na wasiopungua theluthi mbili ya wabunge wote kutoka Zanzibar.
(5) Bila kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (4), Bunge litatunga Kanuni za Kudumu zitakazoweka utaratibu wa-

(a) kuwasilisha, kujadili na kupitisha Muswada wa Sheria; na
(b) utekelezaji bora wa masharti ya ibara ndogo ya (3).
129.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, wananchi watakuwa na haki ya kumwondoa mbunge wao madarakani, endapo mbunge atafanya moja wapo au zaidi ya mambo yafuatayo:
(a) kuunga mkono sera ambazo zinaenda kinyume na masilahi ya wapigakura au kinyume na masilahi ya Taifa;
(b) kushindwa kuwasilisha au kutetea kwa dhati hoja zinazotokana na kero za wapigakura wake;
(c) kuacha kuishi au kuhamisha makazi yake kutoka eneo la Jimbo la Uchaguzi kwa zaidi ya miezi sita bila sababu za msingi; au
(d) mambo mengine yatakayoainishwa kwenye sheria ya nchi.
(2) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya kuendesha uchunguzi kwa Mbunge atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake kwa wapigakura wake na utaratibu wa kumwondoa katika ubunge.
146.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii yanayolinda na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge, ni marufuku kusema uongo bungeni na kwa sababu hiyo, mbunge anapozungumza ndani ya Bunge ana wajibu wa kuhakikisha kwamba anatoa kauli au maelezo kuhusu jambo au suala ambalo yeye mwenyewe anaamini kuwa ni la kweli na siyo jambo la kubuni au la kubahatisha.
(2) Mbunge anapokuwa akizungumza bungeni hatahesabika wala kutafsiriwa kuwa anasema uongo iwapo anafanya rejea ya habari kuhusu jambo lililotangazwa au lililoandikwa na vyombo vya habari au nyaraka nyingine yoyote ambayo chanzo chake kinafahamika au kitaelezwa na mbunge huyo.
231. Vyanzo vya mapato ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano vitakuwa:
(a) ushuru wa bidhaa;

(b) mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na taasisi za Muungano;
(c) mchango kutoka kwa nchi washirika;
(d) mikopo kutoka ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano; na
(e) mapato mengine.
234. Serikali za nchi washirika zitakuwa na benki zitakazokuwa na jukumu la kutunza akaunti ya fedha za Serikali ya nchi mshirika husika, kusimamia sera za kifedha na benki za biashara katika mamlaka zao.
242.-(1) Kutakuwa na Tume ya Utumishi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania itakayokuwa na jukumu la kusimamia masuala yote ya utumishi katika Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.
(2) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu muundo, majukumu na mambo mengine yanayohusu Tume ya Utumishi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.
244.-(1) Katika utekelezaji wa majukumu yake, Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano litazingatia-
(a) viwango vya juu vya kitaaluma na nidhamu miongoni mwa wafanyakazi wake;
(b) ulinzi na ukuzaji wa haki za binadamu;
(c) kanuni za uwazi na uwajibikaji; na
(d) kukuza uhusiano na jamii.

(2) Jeshi la Polisi, katika kutekeleza majukumu yake, litashirikiana na vyombo vinavyohusika na kupambana na uhalifu vya Nchi Washirika katika kufanya uchunguzi na kushughulikia makosa ya rushwa na ufisadi.
246. Mkuu wa Jeshi la Polisi atatekeleza kazi zake kwa uhuru, bila woga, upendeleo wala chuki na kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii na sheria za nchi.
247.-(1) Kutakuwa na Tume ya Utumishi wa Jeshi la Polisi itakayokuwa na jukumu la kusimamia utumishi wa Jeshi la Polisi.
(2) Katika uajiri wa askari wa Jeshi la Polisi, Tume ya Utumishi wa Jeshi la Polisi itazingatia kanuni na misingi ya utumishi iliyoainishwa katika Katiba hii.
(3) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya muundo na utekelezaji wa kazi na majukumu ya Tume ya Utumishi wa Jeshi la Polisi.
250.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Sura hii, Wakuu wa Nchi Washirika wanaweza kumwagiza kiongozi yeyote wa Jeshi la Polisi au Idara ya Usalama wa Taifa kuchukua hatua yoyote ambayo ni muhimu kwa ajili ya kulinda au kuimarisha usalama wa eneo lolote la Nchi Mshirika husika.
(2) Bunge litatunga sheria itakayoainisha masharti yanayohusu namna bora ya utekelezaji wa Ibara ndogo ya (1).
253.-(1) Watumishi wafuatao hawatakuwa na haki ya kugombea, kuchaguliwa au kuteuliwa katika nafasi ya kisiasa hadi utakapopita muda wa miaka mitatu tokea kuacha au kustaafu nafasi ya madaraka aliyokuwa akiishikilia:
(a) Jaji Mkuu, Naibu Jaji Mkuu na Jaji wa Mahakama ya Juu wa Jamhuri ya Muungano;
(b) Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Jaji wa Mahakama ya Rufani;
(c) Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
d) Spika na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;

(e) Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama;
(f) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
(g) Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
(h) Makatibu Wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano; na
(i) Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mkurugenzi wa Uchaguzi;
(j) Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu;
(k) Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume ya Maadili ya Uongozi na Uwajibikaji;
(l) Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Umma;
(m) Msajili wa Vyama vya Siasa.
(2) Bunge linaweza kutunga sheria kuhusu aina nyingine ya watumishi wa umma ambao hawataruhusiwa kushika nafasi za madaraka ya kisiasa kwa mujibu wa Ibara hii.

TANGAZO LA USAILI WA JESHI LA POLISI TANZANIA KWA WAKAZI WA MBEYA.



Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, AHMED Z. MSANGI – SACP anawatangazia Wananchi wote ya kuwa vijana waliomaliza Kidato cha Nne mwaka 2013 na cha Sita mwaka 2014 na kuchaguliwa kufanya usalii wa kujiunga na Jeshi la Polisi, Usaili huo utafanyika kuanzia Tarehe 28.09.2014 hadi Tarehe 01.10.2014 kuanzia majira ya saa 08:00 Asubuhi hadi saa 16:00 jioni katika Shule ya Sekondari Mbeya Day.

Muhimu:

·         Mwombaji aliyeitwa kwenye usaili aje na vyeti vyake vyote vya masomo [(Academic Certificate(s)/Results slip(s) & Leaving certificate(s)], nakala halisi ya cheti cha kuzaliwa (Original Birth certificate). Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.
·         Mwombaji awe na namba ya simu itakayotumika kumjulisha endapo atachaguliwa.
·         Kila mwombaji aliyeitwa kwenye usaili atajigharamia usafiri, chakula na malazi kwa muda wote wa zoezi la usaili. Pia waombaji waje na kalamu za wino kwa ajili ya usaili wa kuandika.

Ni muhimu sana kwa kila mwombaji kuzingatia tarehe ya usaili na muda wa kuanza usaili.

ST. MARCUS SCHOOLS MBEYA; TANGAZO LA NAFASI ZA MASOMO

 KARIBU ST.MARCUS SCHOOLS, ZILIZOPO IWAMBI MBEYA.




 BAADHI YA WANAFUNZI AMBAO WANASOMA KATIKA SHULE YA ST.MARCUS SCHOOLS, ZILIZOPO IWAMBI JIJINI MBEYA. WANALELEWA KATIKA MAZINGIRA MAZURI NA YENYE MAADILI MEMA.
 BAADHI YA WANAFUNZI WA SEKONDARI KATIKA ST,MARCUS SCHOOLS, IWAMBI MBEYA TANZANIA.

SHULE za kisasa za ST. MARCUS NURSERY, PRIMARY AND SECONDARY SCHOOLS, zilizopo Iwambi Jijini Mbeya, zinatangaza nafasi za masomo kwa Nurser, Primary na Sekondari kwa mwaka 2015.
Shule za St. Marcus, ni za kutwa na bweni, kwa wavulana na wasichana wa dini zote, zimesajiliwa kwa mchepuo wa English Medium.
Shule zinatoa huduma mbalimbali, ikiwemo usafiri kwa wanafunzi wanafunzi watokao nyumbani, St. Marcus ina walimu wazoefu, maktaba, darasa la Computer, maabara za kisasa kwa masomo ya sayansi.
St. Marcus Secondary, imeshika nafasi ya pili kitaaluma kwa Jiji la Mbeya, mtihani wa Mock kidato cha pili kwa mwaka 2014.
Kwa wanaohitaji kujiunga, usaili utafanyika Tarehe 11/10/2014 na Tarehe 22/11/2014 saa tatu asubuhi katika maeneo yafuatayo, vituo vya St. Marcus Schools, Mbeya, Ignatus school, Dodoma na Perfect Vission Secondary School, Dar Es Salaam.
Fomu za kujiunga zinapatikana shuleni St. Marcus schools, Mbeya, Rombo Green view Hotel, Dar es Salaam, Martin Luther School, Dodoma, Ofisi za Radio Jogoo, Songea na Kalenga Hotel Iringa Mjini.
Wote mnakaribishwa.
Kwa mawasiliano zaidi piga simu 0764 171742 na 0754 691038
Au tembelea website www.stmarcusschools.ac.tz

Thursday, September 25, 2014

BULAYA ATANGAZA VITA DHIDI YA WASSIRA

Dar es Salaam. Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya ametangaza rasmi nia ya kugombea ubunge katika Jimbo la Bunda ambalo linashikiliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira.
Kwa nia hiyo, Bulaya anaweza kuwa ametangaza vita dhidi ya Wasira ambaye hivi karibuni akiwa Bunda, alitangaza kukitetea kiti chake hicho katika Uchaguzi Mkuu 2015.
Julai 8, mwaka huu Wasira akiwa kwenye kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM wilayani Bunda, alitangaza kuwa atatetea nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu ujao, huku akijigamba kuwa yeye ni “mwarobaini wa matatizo” yanayowakabili wakazi wa jimbo hilo.
Kabla ya kutangaza nia hiyo, mara kadhaa Wasira amekuwa akihusishwa na suala la urais na ni mmoja wa makada sita wa CCM ambao walipewa adhabu na chama hicho Februari 18 mwaka huu, baada ya kukutwa na makosa ya kuanza mapema kampeni za urais mwaka 2015.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili jana, Bulaya alisema atagombea ubunge katika Jimbo la Bunda na anamtakia kila heri mpinzani wake huyo (Wasira) katika nafasi ya juu ya urais anayotaka kuwania. Alisema ameamua kufanya hivyo baada ya kuombwa na watu kadhaa kutoka jimboni humo wakiwamo vijana, wazee na kinamama.
“Ninaamini nimepata uzoefu mkubwa katika kipindi hiki cha ubunge wa viti maalumu na ninawataka wabunge wenzangu wa viti maalumu waone kuwa nafasi hiyo ni fursa ya kujifunza, lakini mwisho wa yote lazima urudi jimboni,” alisema.
“Hii ni mara ya kwanza nasema hapa. Nitagombea ubunge Jimbo la Bunda kwa kuwa nimeombwa sana na vijana, wazee na ni mara nyingi nimekuwa nikisema bado muda, lakini sasa umebaki muda mfupi hivyo niseme tu kwamba nitagombea. Uongozi ni mbio za kupokezana vijiti. Wasira ni kama baba yangu na sina ugomvi naye na namtakia kila la heri katika position (nafasi) yake nyingine anayoitaka,” alisema.
Kuhusu madai kwamba Wasira anafikiria kuwania urais, alisema, “Naona ni uamuzi sahihi amefanya, kwani amekuwa mbunge tangu mimi nazaliwa mwaka 1980 ameona kwamba ni kweli hii position (nafasi) ya chini ameshaitumikia sana, hivyo ameona katika uzoefu alionao labda ajaribu katika nafasi ya urais.”
Bulaya alisema si kwamba ameamua kugombea ubunge wa Bunda kwa kuwa Wasira anataka urais, bali viti maalumu alipo hivi sasa ni njia ya kupata uzoefu na kujifunza katika kuelekea kugombea ubunge wa jimbo.
“Ili kuondoa suala la kwamba viti maalumu ni vya kupewa siyo kwamba nasema vifutwe, lakini unaweza ukawekwa utaratibu mwingine wa kumpa mwanamke uzoefu katika ngazi ya kibunge,” alisema na kuongeza;
“Lakini unapopewa hebu itendee haki hiyo fursa, kama mtu umeingia viti maalumu unajifunza na unakwenda kugombea na huko kuna kushinda na kushindwa lakini ni lazima nionyeshe hii fursa nimepewa naweza kwenda kushindana na wanaume.”
Alisema hilo ni jambo la msingi kwa kuwa huwezi kulemaa kwa kuwa mbunge wa viti maalumu bila kujifunza na kukaa miaka hadi 15 kwenye ubunge wa aina hiyohiyo kwani wako wengine wanaotakiwa kupata nafasi hiyo ili wajifunze na kwenda majimboni.

HII NDIYO RASIMU MPYA YA KATIBA NA MAMBO YOTE YA MSINGI!!!

Dodoma. 
 Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba jana ilikabidhi bungeni Rasimu ya Katiba inayopendekezwa ikiwa na ibara 289 kulinganisha na 271 za Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Warioba.
Rasimu hiyo pia ina sura mpya mbili ambazo ni Mamlaka na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na nyingine inayohusu Ardhi, Maliasili na Mazingira.
Akiwasilisha rasimu hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Andrew Chenge aliliambia Bunge kuwa Ibara 233 za rasimu hiyo zinatokana na Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Chenge, ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), alisema ibara 47 za Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba zimebaki kama zilivyokuwa, 186 zimefanyiwa marekebisho, 28 zimefutwa na 41 ni mpya.
Rasimu hiyo ya Katiba inayopendekezwa imefuta kabisa muundo wa Muungano wa shirikisho ambao ungezaa muundo wa serikali tatu na badala yake imerudisha muundo wa sasa wa serikali mbili.
Chenge alisema kamati za Bunge hilo pamoja na wajumbe walio wengi, waliona kuingiza muundo wa shirikisho ilikuwa ni kukiuka makubaliano ya Muungano yaliyofikiwa mwaka 1964.
Kwa kurejesha muundo wa serikali mbili uliokuwa ukipigiwa chapuo na CCM, Rasimu hiyo imependekeza kuwapo kwa makamu watatu wa rais.
Chenge alisema uongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mgombea mwenza atakayekuwa makamu wa kwanza wa rais.
Chini ya muundo huo, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), atakuwa makamu wa pili wa rais ilhali Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakuwa makamu wa tatu wa rais.
Chenge alisema mapendekezo hayo yamezingatia ukweli kuwa kuwapo kwa mgombea mwenza anayekuwa makamu wa kwanza wa rais, kutafanya rais na makamu wake kutoka chama kimoja.
Rasimu hiyo inayopendekezwa, imepunguza Tunu za Taifa kutoka saba zilizokuwamo kwenye Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba hadi nne huku mambo ya muungano yakiongezwa kutoka saba hadi 14.
Katika Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Tunu za Taifa zilikuwa ni utu, uzalendo, uadilifu, umoja, uwazi, uwajibikaji na lugha ya Taifa; sasa zimebaki Lugha ya Kiswahili, Muungano, utu na undugu na amani na utulivu. Tunu tatu ambazo ni uzalendo, uadilifu na umoja zimeondolewa.

Mambo ya Muungano
Katika Rasimu ya Tume, mambo ya Muungano yaliyoorodheshwa ni Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ulinzi na usalama.
Mambo mengine yalikuwa ni uraia na uhamiaji, sarafu na benki kuu, mambo ya nje, usajili wa vyama vya siasa, ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano.
Rasimu inayopendekezwa imetaja mambo ya muungano kuwa ni Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ulinzi na usalama, usafiri wa anga, uraia, uhamiaji, polisi, sarafu na benki kuu na kodi ya mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na bidhaa zinazotengenezwa Tanzania na kusimamiwa na idara ya forodha.
Mengine ni mambo ya nje, usajili wa vyama vya siasa, Mahakama ya Juu na Mahakama ya Rufani, elimu ya juu, Baraza la Taifa la Mitihani, Utabiri wa Hali ya Hewa na utumishi Serikali ya Jamhuri.
Mambo mengine ambayo yalikuwa katika Rasimu ya Warioba yaliyowekwa kando ni pendekezo la wabunge kutokuwa mawaziri ikipendekezwa utaratibu wa sasa wa wabunge kuwa mawaziri uendelee kutumika.
Chenge alisema Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, imeweka ukomo wa mawaziri kuwa wasizidi 30 wakati naibu mawaziri watateuliwa kulingana na mahitaji mahsusi. Tume ya Warioba ilipendekeza mawaziri wasiozidi 15.
Rasimu hiyo inayopendekezwa imefumua muundo wa Bunge uliopendekezwa na Rasimu ya Warioba kuwa wawe 75 wa kuchaguliwa majimboni na watano kutoka kundi la watu wenye ulemavu, badala yake imesema muundo wa sasa uendelee ukiwa na wabunge 360 kwa sharti la kuwapo uwiano sawa kati ya wanawake na wanaume.
Rasimu hiyo imetupilia mbali pendekezo la mtu anayetaka kugombea ubunge awe na elimu isiyopungua kidato cha nne na kurudisha kuwa ajue tu kusoma na kuandika Kiswahili au Kiingereza.
“Haki ya wananchi kumwajibisha mbunge kabla ya miaka mitano imeondolewa kutokana na mapendekezo ya kamati na wajumbe na watafanya hivyo baada ya miaka mitano,” alisema.
Rasimu hiyo imembana mgombea binafsi wa ubunge kwamba atakoma kuwa mbunge pale tu itakapotokea amejiunga na chama chochote cha siasa nchini.

Pendekezo la Warioba la kutaka Spika wa Bunge na Naibu wake wasitokane na wabunge wa Bunge la Jamhuri au kuwa viongozi wa juu wa vyama, nalo limewekwa kando na badala yake spika kupendekezwa achaguliwe miongoni mwa wabunge au kutoka kwa Watanzania wenye sifa ambao watajitokeza kuomba nafasi hiyo kama ilivyo sasa.
Hata hivyo, Chenge alisema wamependekeza Naibu Spika ni lazima atoke miongoni mwa wabunge.
Mgombea binafsi
Chenge alisema pamoja na kwamba mgombea huru wa nafasi ya urais ni haki ya kikatiba, lakini kamati yake imelazimika kuchukua tahadhari na kuweka masharti juu ya mgombea huyo.
Masharti hayo ni pamoja na kuweka kipengele katika Katiba kinacholitaka Bunge kutunga sheria itakayoweka masharti ya mgombea huru ikiwamo idadi ya watu watakaohitajika kumdhamini.
Pia sheria hiyo itaweka sharti la lazima linalomzuia kujiunga na chama chochote cha siasa, kuainisha vyanzo vya mapato vya kugharimia kampeni zake na kuweka wazi ilani yake ya uchaguzi.
Masuala ya kuingizwa kwa Mahakama ya Kadhi na kuruhusiwa kwa uraia wa nchi mbili ambayo yaliwagawa wajumbe wa Bunge hilo katika makundi mawili nayo hayakuingizwa katika rasimu hiyo.
Kuhusu Mahakama ya Kadhi, Chenge alisema kamati yake imezingatia mijadala ya wajumbe, taarifa za kamati za Bunge hilo na Katiba za nchi mbalimbali katika kufikia uamuzi huo.
Alisema katiba inayotungwa inahusu Mahakama Kuu, Mahakama ya Rufani na Mahakama ya Juu hivyo masuala ya Mahakama ya Kadhi yanaweza kusimamiwa na sheria inayohusu mahakimu.
Kuhusu suala la uraia pacha, Chenge alisema waliozaliwa Tanzania lakini wakapoteza uraia na kuamua baadaye kurudi nchini, watarejeshewa uraia wao baada ya kuukana uraia wa nje. Alisema Watanzania wanaoishi nje ya nchi wakiwa na uraia wa nchi hizo, watakapokuja nchini hawatakuwa na uraia wa nchi mbili, badala yake watapewa hadhi maalumu.
Baada ya kukamilika kwa uwasilishaji huo, Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta alitoa fursa kwa wajumbe wa Bunge hilo kuipitia Rasimu jioni na leo watakutana kwenye kamati zao 12 kwa lengo la kuhakiki ni kwa kiasi gani waliyoyapendekeza wakiwa ndani ya kamati na kwenye mijadala yamezingatiwa.
Kesho wajumbe wote watakutana katika Bunge zima kwa lengo la kuhakiki kwa pamoja kuhusu yale yatakayoletwa na sekretarieti kutoka kwenye kamati za Bunge hilo. Septemba 28, wajumbe hao watakutana tena kwenye kamati kwa lengo la kupewa maelekezo ya namna ya kukaa ndani ya ukumbi na pia namna watakavyopiga kura siku inayofuata.
 Sitta alisema upigaji wa kura utaanza Septemba 29 hadi Oktoba 2 na baada ya hapo itajulikana kama rasimu hiyo imepitishwa kwa wingi wa kura wa theluthi mbili kwa pande zote za Muungano au la.

Monday, September 22, 2014

KESI YA MBASHA YASOGEZWA MBELE TENA!!

Kesi ya mwimbaji wa nyimbo za Injili Emmanuel Mbasha imepigwa kalenda kwa mara nyingine tena kwa sababu Hakimu anayeendesha kesi hiyo kupata shughuli nyingine nje ya ofisi.Mbasha alipanda kizimbani katika mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi yake hiyo ambapo mwendesha mashtaka Kiyoja Catherine aliahirisha kesi hiyo kutokana na Hakimu Williberforce Luwhego kupata dharura.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena 17 October mwaka huu ambapo Mahakama itaanza kusikiliza ushahidi ambapo upande wa mashtaka utakuwa na mashahidi wanne kwenye kesi hii inayomkabili mume wa Flora Mbasha anaekabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo ya ubakaji. 
Mara ya mwisho kabla ya hii kuahirishwa Flora Mbasha alikwenda Mahakamani kwa mara ya kwanza akiwa na watu wake na hakukutana wala kuongea na mume wake ambapo muda mfupi kesi hiyo ikaahirishwa.

WAREMBO MISS TANZANIA WATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA MIKUMI!!!

Warembo 30 wanaoshiriki shindano la Redd's Miss Tanzania 2014 jana walitembelea hifadhi ya taifa ya Mikumi mkoani Morogoro kujionea vivutio mbalimbali vya utalii viliovyopo katika hifadhi hiyo ambapo waliweza kujionea wanyama wa aina mbalimbali wakiwepo, Tembo, Twiga, Swala, Viboko na Simba.
 Kaimu Mhifadhi Utalii wa Hifadhi ya Taifa Mikumi, Apaikunda Mungure akigawa vipeperushi kwa warembo.
Warembo walibahatika kuwaona Simba zaidi ya Saba wakiwamepumzika chini ya mti.
 Warembo wa Redd's Miss Tanzania wakiongozwa na Matron wao, Gladness Chuwa mbugani Mikumi.

Warembo wakipiga picha na watalii waliowakuta Mikumi.


 Punda milia nao walionekana kwa wingi.
 Wakisikiliza maelezo juu ya Viboko kutoka kwa Benina Mwananzila.
 Warembo wakipata maelezo katika kituo cha Mbuyu
 Muongoza watalii Ibrahim Kassim akitoa maelezo kwa washiriki wa shindano la Redd's Miss Tanzania 2014.
 Mrembo akitazamana na ngedere
 Warembo wakitembelea lodge ya Hifadhi hiyo ya Mikumi.
 Tembo nao walikuwepo.
 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA POLISI TANZANIA.




 
RPC.                                                                                               Ofisi ya Kamanda wa Polisi,                                                                                                                                                                                                                                                                                               Mkoa wa Mbeya,                                                                                    
Namba ya simu 2502572                                                                                         S. L. P. 260,
Fax - +255252503734                                                                                                 MBEYA.
E-mail:-  rpc.mbeya@tpf.go.tz                                                                      


KATIKA TUKIO LA KWANZA:

MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA 08 ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA ANITHA SHARIFU MWANAFUNZI WA DARASA LA PILI KATIKA SHULE YA MSINGI NKANGAMO ALIFARIKI DUNIA AKIWA ANAOGELEA KATIKA MTO ILUMA ULIOPO WILAYANI MOMBA.

TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 20.09.2014 MAJIRA YA SAA 18:30 JIONI HUKO KATIKA KIJIJI CHA NDALAMBO, KATA NA TARAFA YA NDALAMBO, WILAYA YA MOMBA, MKOA MBEYA. INADAIWA KUWA MTOTO HUYO ALIZIDIWA NA MAJI YA MTO HUO HALI IYOPELEKEA KUZAMA NA KUSABABISHA KIFO CHAKE.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA WAZAZI/WALEZI KUWA MAKINI NA WATOTO WADOGO, KUTOWARUHUSU KWENDA KUOGELEA HAMA KUKARIBIA MAENEO YENYE MAJI KAMA MITO NA MABWAWA YENYE MAJI KWANI NI HATARI KWA WATOTO.


KATIKA MSAKO:

JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WATATU RAIA NA WAKAZI WA NCHINI ETHIOPIA AMBAO NI 1. SHUGUTI SHIMACHO (30) 2. AWADHI SULEIMAN (27) na 3. TAKATARI AYELE (20) KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI.

WATUHUMIWA HAO WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 21.09.2014 MAJIRA YA SAA 20:54 USIKU HUKO MAENEO YA STENDI KUU YA MABASI TUKUYU MJINI, KATA YA KAWETELE, TARAFA YA TUKUYU MJINI, WILAYA YA RUNGWE, MKOA WA MBEYA. TARATIBU ZA KUWAKABIDHI IDARA YA UHAMIAJI KWA TARATIBU ZAIDI ZA KISHERIA ZINAENDELEA.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA WANANCHI KUENDELEA KUTOA TAARIFA ZA MTU/WATU WANAOWATILIA MASHAKA KATIKA MAENEO YAO ILI UCHUNGUZI DHIDI YAO UFANYIKE. AIDHA, ANATOA WITO KWA WAGENI KUFUATA TARATIBU ZILIZOWEKWA ZA KUINGIA NCHINI KWANI KUTOFANYA HIVYO NI KINYUME CHA SHERIA.


Imesainiwa na:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

HAYA JAMANI NAFASI ZA KAZI HIZO!





NAFAZI ZA KAZI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 15 /10/2014


NAFASI ZA AJIRA JESHI LA MAGEREZA - 20 / 9 /2014
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
(Jeshi la Magereza)
TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA
Jeshi la Magereza Tanzania Bara linatangaza nafasi za Mafunzo ya Awali ya Askari Magereza yatakayoendeshwa Chuo cha Magereza Kiwira Tukuyu Mbeya. Waombaji wa nafasi hizo wanatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-

MASHARTI YA KUAJIRIWA:
1. JINSI: Mvulana au Msichana ambaye hajawahi kuoa au kuolewa na asiwe na mtoto
2. URAIA: Awe Raia wa Tanzania Bara

3. UMRI: (a) Wahitimu wa Shahada: Awe na umri wa kati ya miaka 18 na 28 (b) Wasio na Shahada: Awe na umri wa kati ya miaka 18 na 24

4. UREFU:
(a) Wavulana: Wawe na urefu usiopungua Sentimeta 170.2 au Futi
5 na inchi 7
(b) Wasichana: Wawe na urefu usiopungua Sentimeta 167.64 au
Futi 5 na inchi 4

5. SIFA NYINGINEZO:
i) Awe amehitimu Elimu yake kati ya Mwaka 2012 na 2014
ii) Awe na Afya nzuri iliyothibitishwa na Daktari anayetambuliwa na Serikali
iii) Awe hajawahi kushtakiwa wala kupatikana kwa kosa lolote la jinai
iv) Awe na tabia na mwenendo mzuri
v) Awe hajawahi kuajiriwa mahali popote Serikalini

7. ELIMU:
(A) WENYE SHAHADA KATIKA FANI AU TAALUMA ZIFUATAZO:
(I) SHAHADA YA SHERIA (LAWS)
(II) UTEKELEZAJI WA SHERIA (LAW ENFORCEMENT)
(III) TAKWIMU (APPLIED STATISTICS)
(IV) UCHUMI NA MIPANGO (ECONOMIC PLANNING)
(V) MAZINGIRA (ENVIRONMENTAL SCIENCE AND MANAGEMENT OR GEOGRAPHY AND ENVIRONMENT STUDIES)
(VI) USANIFU MAJENGO (ARCHITECTURE)
(VII) UKADIRIAJI MAJENGO (BUILDING ECONOMICS)
(VIII) MIPANGO NA USIMAMIZI MIRADI (PROJECT PLANNING AND MANAGEMENT)
(IX) UHANDISI WA UMEME (ELECTRICAL ENGINEERING)
(X) UHANDISI WA MITAMBO YA KILIMO (AGRICULTURAL ENGINEERING)
(XI) TIBA YA MIFUGO (VETERINARY MEDICINE)
(XII) MISITU (FORESTRY)
(XIII) UCHUMI KILIMO (AGRONOMY)
(XIV) BIMA (INSURANCE)
(XV) UHASIBU NA USIMAMIZI WA VYAMA USHIRIKA (COOPERATIVE MANAGEMENT AND ACCOUNTANCY)
(XVI) (PROJECT PLANNING AND MANAGEMENT)
(XVII) UHANDISI MAZINGIRA (ENVIRONMENTAL ENGINEERING)
(XVIII) SAYANSI YA KOMPYUTA (COMPUTER SCIENCE)
(XIX) UDAKTARI WA BINADAMU (DOCTOR OF MEDICINE)
(XX) UALIMU WA MASOMO YA SAYANSI KAMA FIZIKIA, KEMIA, BAIOLOJIA NA HISABATI
(XXI) UALIMU WA MASOMO YA BIASHARA NA KIFARANSA (COMMERCIAL SUBJECTS, ECONOMICS AND FRENCH)
(XXII) UKUTUBI (LIBRARY AND INFORMATION STUDIES)
(XXIII) MAHUSIANO (PUBLIC RELATIONS)
(XXIV) BIASHARA NA MASOKO (COMMERCE IN MARKETING)

(B) WASIO NA SHAHADA
1.1: WENYE STASHAHADA (DIPLOMA) TOKA KATIKA VYUO VINAVYOTAMBULIWA NA SERIKALI KATIKA FANI/TAALUMA ZIFUATAZO:-
(I)UKUTUBI (LIBRARY)
(II) UCHUMI NA MIPANGO (ECONOMIC PLANNING)
(III) BIMA (INSURANCE)
(IV)UHASIBU NA USIMAMIZI WA VYAMA USHIRIKA (CO-OPERATIVE MANAGEMENT AND ACCOUNTANCY)
(V)MIPANGO NA USIMAMIZI MIRADI (PROJECT PLANNING AND MANAGEMENT)
(VI)UTABIBU (CLINICAL MEDICINE)
(VII)UUGUZI (NURSING)
(VIII)MAABARA (LABORATORY TECHNICIAN)
(IX)MAZOEZI YA VIUNGO (PHYSIOTHERAPY)
(X) UANDISHI WA HABARI (JOURNALISM)
(XI)UFUNDI MAGARI (AUTOMOBILE TECHNICIAN)
(XII) UJENZI (CIVIL ENGINEERING)
(IX) UMWAGILIAJI (IRRIGATION)
(X) MITAMBO YA KILIMO (AGRO-MECHANICS)
(XI)UMEME (ELECTRICAL ENGINEERING)
(XII) USANIFU MAJENGO (ARCHITECTURE)
(XIII) USHAURI NASAHA (COUNSELING AND GUIDANCE)
(XIV)UHANDISI MITAMBO (MECHANICAL ENGINEERING)
(XV)SANAA NA MUZIKI (FINE AND PERFORMING ARTS)
(XVI)UALIMU WA MASOMO YA BIASHARA, UCHUMI NA KIFARANSA

1.2: WENYE ASTASHAHADA/ CHETI CHA MAJARIBIO YA UFUNDI KATIKA FANI/TAALUMA ZIFUATAZO:-
(I) UHANDISI MAJI (WATER ENGINEERING)
(II) UJENZI (MASONRY)
(III) UFUNDI MAGARI (MOTOR VEHICLE MECHANICS)
(IV) UMEME WA MAGARI (AUTO-ELECTRICAL ENGINEERING)
(V) WAUNGANISHAJI NONDO (STEEL FIXING)
(VI) USEREMALA (CARPENTRY AND JOINERY)
(VII) BOMBA (PLUMBING AND PIPE FITTING)
(VIII) RANGI (SPRAY AND PAINTING)
(IX) USHONAJI (TAILORING)
(X) UTENGENEZAJI SABUNI (SOAP MAKING)
(XI) UFUMAJI (EMBROIDERY)
(XII) KUTENGENEZA VIATU (SHOE-MAKING)
(XIII) MAABARA (LABORATORY TECHNICIAN)
(XIV) UHITASI (SECRETARIAL STUDIES WITH COMPUTER KNOWLEDGE)
(XV) MUZIKI NA UTAMADUNI (PERFORMING ARTS AND MUSIC)
(XVI) UUGUZI NA UKUNGA (NURSING AND MIDWIFE)
(XVII) UTABIBU USAIDIZI (CLINICAL ASSISTANT)

ZINGATIO:
Waombaji wa nafasi hizi wahakikishe wanazingatia masharti yote yaliyotajwa hapo juu. Upungufu au udanganyifu wowote utakaojitokeza kwa kutotimiza masharti yaliyotajwa hapo juu utasababisha maombi kutopokelewa na ikigundulika baada ya ajira mhusika atasitishwa mafunzo, kuachishwa kazi na kufikishwa Mahakamani.

8. NAMNA YA KUTUMA MAOMBI:

Waombaji wote watume maombi yao moja kwa moja kwa:-

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA,
MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA,
S.L.P 9190,
DAR ES SALAAM.

a) Barua zote za maombi ziambatane na nakala za vyeti vyote vya elimu, ujuzi, Cheti cha kuzaliwa mwombaji na picha ndogo ya hivi karibuni ya mwombaji (Passport size photograph). Vyeti halisi na halali vitatakiwa kuoneshwa wakati wa usaili. Hati za matokeo ya mitihani (Results Slip/ Statement) hazitakubaliwa isipokuwa kwa wahitimu ambao vyeti vyao halisi havijatolewa na Vyuo husika pekee.

b) Watakaofanikiwa kuitwa kwenye usaili watajulishwa kupitia katika Tovuti ya Jeshi la Magereza (www.magereza.go.tz), Magazeti na katika Mbao za matangazo zilizopo kwenye Ofizi za Wakuu wa Magereza wa Mikoa na Bwalo Kuu la Maafisa wa Magereza lililopo Ukonga Dar es salaam.
c) Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 15 Oktoba, 2014.







NAFASI ZA KAZI MASAKAMALI INSTITUTE OF BUSINESS MWISHO WA WA KUTUMA MAOMBI TAR 30 SEPT 2014




THE LEGAL SERVICES FACILITY IS AN INDEPENDENT BASKET FUND

SUPPORTED BY DANIDA AND UKAID
JOB OPPORTUNITIES
The Legal Services Facility (LSF) offers a fast growing, high performance working environment which provides support for the enhancement of legal aid and legal empowerment in Tanzania, with emphasis on the protection of women’s rights. Through 47 implementing partners, the LSF presently funds in all districts of Tanzania the setting up or improvement of basic legal aid services.
Additionally the fund is involved in and supports capacity development of legal aid providers, advocacy for recognition of paralegals through legal aid legislation, innovative approaches to legal aid and increasing awareness about the importance of legal aid and legal empowerment in the development process.
The LSF is an equal opportunity employer and invites both women and men, who think they fulfil the requirements and who are willing to go the extra mile, to apply.

OPERATIONS AND LEARNING MANAGER
The O&L Mamager will oversee the implementation of LSF strategies developed, will contribute to the formulation of medium term results and their measurement, will oversee an extensive pilot project and will execute other managerial tasks. The position is based at the LSF office in Dar es Salaam and reports to the CEO/Fund Manager. Candidates need to be at least available for the period from 1 October 2014 to 31 December 2015.
The position in particular includes:

• Formulation of essential result components in grant making and grant management;

• Effective improvement and implementation of a more comprehensive Monitoring and Results System that includes outcome mapping and qualitative data sourcing and recording;

• Conceptualising and implementing legal empowerment;

• Conceptualising and implementing the development of the LSF and implementing partners towards increasingly becoming learning organisations;

• Substantially contribute to LSF reporting and dissemination of lessons learned;

• Maintaining and building networks and develop and maintain communication.

Additionally, the position will oversee a pilot project that is implemented in different parts of the country by 4 partners. The pilot is to provide essential learning components for the LSF program as regards the dynamics between paralegal service delivery and local government authorities, including law and order and justice systems. The pilot will also be instrumental toward institutionalising learning within the LSF and within the partner organisations for national scale implementation of a legal empowerment approach.
All tasks are to be implemented in close cooperation with the Fund Manager and other team members in the LSF.
Requirements:
General Qualifications:

• Masters in law, social sciences or similar, from a recognised university;

• More than 10 years’ experience working in increasingly senior positions in international development programmes, preferably in legal sector reform, legal empowerment, paralegal operations, results management and organisational learning.

Specific Qualifications

• Extensive experience in management and running of grant making programs targeting CSOs, preferably in the legal sector;

• Extensive experience from Eastern Africa, in particular Tanzania;

• Extensive experience working with NGOs and CSOs as well as (local) governments;

• Good knowledge of international standard M&E systems (including outcome mapping);

• Good knowledge of communication/dissemination/PR. Excellent (report) writing skills;

• Knowledge of HRBA and processes of change is considered an advantage.

• Fluency in English and Kiswahili

How to apply ?
If you think you are qualified for and interested in the above positions, then please send, or, preferably, hand deliver in an envelope on which the position for which you apply is written and which at least contains:
your printed and signed application letter, CV, copies of certificates and the names of three referees to the address below:
Fund Manager
Legal Services Facility
Bima Street, Nyati Rd, Mikocheni B
P.O.Box 31480
Dar es Salaam, Tanzania Tel: 0222 781061
There is no need for candidates, who have applied earlier for this position, to present their application again.
The deadline for receipt of applications is Monday 29 September 2014 at 4:00 p.m. 3
SOURCE DAILY NEWS OF 22 SEPTEMBER 2014.



NAFASI YA KAZI WIZARA YA KILIMO NA CHAKULA MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 10/10/2014


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA MINISTRY OF AGRICULTURE, FOOD SECURITY AND CO-OPERATIVES RUFIJI BASIN DEVELOPMENT AUTHORIY- RUBADA


CURRENTLY, RUBADA IS ADVERTISED FOR THE POSITION OF DIRECTOR GENERAL.
1. REQUIRED QUALIFICATIONS: The applicant must be holder master’s degree in economics, public administration business, administration, agricultural economics, law or equivalent. The applicant must have 12 years of proven experience of which 8 years’ experience should have been at a sernior managerial position in a reputable organization. The applicant should also have a long experience with government/ civil service.


2. DUTIES AND RESPONSIBILITY OF DIRECT GENERAL :
• Serve as liaison between the board of directors and the directorates of the authority in handling matters of interested to the board.
• Coordinates the execution of programs, policies and decision which the board of directors approves or adopts.
• Originate and / approves finance and administrative control to ensure integrated execution of RUBADA programs.
• Serves as accounting office to ensure timely submission and approval of the annual budget. Budget executions and timely preparation of annual financial report to stake holders.
• Interpret board instruction to the directors.
• Report to the board on the overall efficiency, effectiveness and economy of RUBADA operations.
• Develops formal definition and communication of RUBADA programs, policies, procedures, and continued delegation of authority and responsibility.


DESIRE ATTRIBUTION AND COMPETENCES
• Must be innovative and result oriented
• Must have ability to maintain a malt- task focus.
• Must be visionary, proactive and forward looking.
• Must demonstrate integrity and professionalism.
• Must be able to deal effectively with demanding situations and to respond with speed.
• Must be able to work independently and under tight time schedules.
• Must able to manage continuity, change and transition.


REMUNERATION:
• She/he will be paid an attractive package as per RUBADA scheme of service PGSS 21 respective retention scheme.
GENERAL CONDITIONS:
• All applicants must be citizen of Tanzania and not above 50 years old.
• Applicants must attach an up to date curriculum vitae (CV) with reliable contacts, postal address, email and telephones numbers.

• Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
• Applicants must attract detailed relevant certified copies of academic certificates:
i. Postgraduate/ degree/advanced diploma/diploma/certificates.
ii. Postgraduate/ degree/advanced diploma/ diploma transcripts.
iii. Form vi and form vi national examination certificates.
iv. Profession certificate from respective boards.
v. One recent passport size picture and birth certificate.
• Presentation of forged academic certificate and other information in the CV will necessitate legal action.
• Applicants who have/ were retired from the public service for whatever reason should not apply
• Applicants should three reputable referees with their reliable contacts.

• Deadline for application is 10 october 2014 at 3: 30 AM
• Short listed candidates will be informed on the date for interview.

APPLICATION LETTERS SHOULD BE POSTED TO THE FALLOWING ADDRESS. HAND DELIVERY IS NOT ACCEPTABLE:
The chair of the board of directors,
Rufiji basin development authority,
RUBADA building, 2nd floor, behind ubungo plaza building, morogoro road,
P.O.BOX 9320
DAR ES SALAAM.
SOURCE: DAILY NEWS OF 22 SEPTEMBER



 NAFASI ZA KAZI MASAKAMALI INSTITUTE OF BUSINESS MWISHO WA WA KUTUMA MAOMBI TAR 30 SEPT 2014



MASAKAMALI INSTITUTE OF BUSINESS
STUDIES AND TECHNOLOGY
TEL: + 255 754 310 149
+255 687 465 262
FAX + 255 732 978 903
info@mitst.ac.tz;
www.mibst ac.tz
REG/BMG/049P

TEACHING OPPORTUNITIES
Msakamali institute of business studies and technology ( MIBST) AN UPCOMING TRAINING INSTITUTION BASED IN MSATA, Bagamoyo District invites application to fill vacant teaching positions in accounting and community development studies.

A. ACCOUNTING STUDIES
Graduate in B.com; ADA or equivalent qualifications.
Applications should be addressed to the managing Director on the above address or emailed to msakamali@yahoo.com
Deadline 30 September 2014
MIBST is an equal opportunity employer and will offer a good package to the successful candidates.
P.O.BOX163, CHALINZE-
TANZANIA
Source: Daily news of 22 September 2014
=============

B. COMMUNITY DEVELOPMENT STUDIES
Degree or advanced Diploma in community Development

Applications should be addressed to the managing Director on the above address or emailed to msakamali@yahoo.com
Deadline 30 September 2014
MIBST is an equal opportunity employer and will offer a good package to the successful candidates.
P.O.BOX163, CHALINZE-
TANZANIA
Source: Daily news of 22 September 2014

Recent Posts


Unordered List