Monday, September 15, 2014

*JAJA AWANYAMAZISHA WANAOMBEZA, YANGA IKIILAMBISHA AZAM ICE CREAM 3-0!!!!

 Jajaaaaaa, mshambuliaji wa Yanga, Jenilson Santos (jaja) akijikunja kupiga mpira wa krosi mbele ya beki wa Azam fc, Erasto Nyoni, wakati wa mchezo wa Ngao ya Jamii uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo jioni.
Katika mchezo huo Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 3-0, huku mabao mawili yakifungwa na jaja aliyefunga bao la kwanza kwa kuunganisha krosi murua ya Simon Msuva na la pili akimchungulia kipa wa Azam fc, Mwadini Ali. 
Bao la tatu lilifungwa na Simon Msuva, ambaye alimpiga kanzu kipa Mwadini Ali na kubaki yeye na goli na kisha kutupia katika nyavu ndogo.
 Jaja, akishangilia bao lake la kwanza na kuwaacha wachezaji wa Azam hoi wasijue la kufanya.
 Jaja akishangilia huku mwamuzi wa mchezo huko, akiwa nyuma yake akionekana kama anamuunga mkono, lakini hapa alikuwa akiwarudisha uwanjani wachezaji hao.
 Wachezaji wa Yanga wakimpongeza mwenzao Jaja baada ya kutupia bao la pili.
 Simon Msuva (kushoto) na Mrisho Ngassa, wakimsapoti Jaja kushangilia bao lake kwa kumfundisha kucheza song la mdogo mdogo.
 Hilo ndo bao la kwanza la jaja.
 Hapa jaja akijaribu kuwatoka mabeki wa Azam fc (msitu).
 Jaja, akimfinya beki wa Azam, Agrey Morris.
 Jaja akiruka kuwania mpira na beki wa Azam, Himidi Mao.
Jaja akipewa medali na wachezaji wenzake wakati wakikabidhiwa zawadi yao ya Ngao ya Hisani baadda ya kuifunga Azam 3-0. HILI NI TOLEO MAALUM LA KUONYESHA KAZI ALIYOIFANYA MCHEZAJI HUYU ALIYEKUWA AKIBEZWA NA KUZOMEWA KILA ALIPOKUWA AKIGUSA MPIRA, KWA MATUKIO ZAIDI YA PICHA ZA MCHEZO HUU ZITAWAJIA BAADAYE, KAA NASI.

0 comments:

Recent Posts


Unordered List